ذَٰلِكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهِ إِلَيۡكَۚ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يُلۡقُونَ أَقۡلَٰمَهُمۡ أَيُّهُمۡ يَكۡفُلُ مَرۡيَمَ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ
Hizi ni khabari za ghaibu tunazo kufunulia; nawe hukuwa nao walipo kuwa wakitupa kalamu zao nani wao atamlea Maryamu, na hukuwa nao walipo kuwa wakishindana.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hizo tulizokusimulia, ewe Mtume, ni miongoni mwa habari za ghaibu alizokujulisha Mwenyezi Mungu kwa njia ya wahyi. Kwani wewe hukuwa pamoja na wao walipotafautiana juu ya nani mwenye haki zaidi na anayefaa kumlea Maryam, ukatokea utesi baina yao, wakapiga kura kwa kuzitupa kalamu zao, ikamwangukia Zakariyyā akapata ushindi wa kumlea.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس