إِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَىٰٓ إِنِّي مُتَوَفِّيكَ وَرَافِعُكَ إِلَيَّ وَمُطَهِّرُكَ مِنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَجَاعِلُ ٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوكَ فَوۡقَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ ثُمَّ إِلَيَّ مَرۡجِعُكُمۡ فَأَحۡكُمُ بَيۡنَكُمۡ فِيمَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ
Pale Mwenyezi Mungu alipo sema: Ewe Isa! Mimi nitakufisha, na nitakunyanyua kwangu, na nitakutakasa na wale walio kufuru, na nitawaweka wale walio kufuata juu ya wale walio kufuru, mpaka Siku ya Kiyama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu, nikuhukumuni katika yale mliyo kuwa mkikhitalifiana.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na vitimbi vya Mwenyezi Mungu kwao ni pale Aliposema Mwenyezi Mungu kumaambia 'Īsā, «Mimi nitakutwaa kutoka kwenye ardhi bila ya kupatikana na baya lolote, nitakuinua mpaka kwangu kwa mwili wako na roho yako, nitakuokoa na watu waliokukanusha na nitawafanya wale waliokufuata wewe, yaani,waliyo kwenye dini yako, na kufuata yale uliyokuja nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu ya dini na bishara ya Mtume Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wakamuamini Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, baada ya kutumilizwa kwake, wakashikamana na Sheria aliyokuja nayo, wawe na ushindi juu ya wale walioukanusha utume wako hadi Siku ya Kiyama; kisha mwisho wenu nyote mtarudi kwangu Siku ya Hesabu, ili nitoe uamuzi juu ya tafauti mliokuwa nazo kuhusu 'Īsā, amani imshukie.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس