فَأَمَّا ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَأُعَذِّبُهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمَا لَهُم مِّن نَّـٰصِرِينَ
Ama wale walio kufuru, nitawaadhibu adhabu kali katika dunia na Akhera, wala hawatapata wa kuwanusuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Ama wale waliomkanusha al- Masīḥ miongoni mwa Mayahudi, au wakamzidishia sifa miongoni mwa Wanaswara, nitawaadhibu adhabu kali katika ulimwengu: kwa kuuawa, kunyang’anywa mali na kuondolewa ufalme, na katika Akhera kwa Moto; na hawatakuwa na msaidizi mwenye kuwanusuru na kuwaepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس