وَدَّت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَوۡ يُضِلُّونَكُمۡ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ
Kipo kikundi katika Watu wa Kitabu wanao penda kukupotezeni; lakini hawapotezi ila nafsi zao, nao wenyewe hawatambui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lilitamani kundi la Mayahudi na Manaswara lau wangaliwapoteza nyinyi, enyi Waislamu, wakawatoa kwenye Uislamu. Wao hawampotezi yoyote isipokuwa nafsi zao na wafuasi wao; na wao hawalielewi hilo wala hawalijui.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس