وَقَالَت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ ءَامِنُواْ بِٱلَّذِيٓ أُنزِلَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَجۡهَ ٱلنَّهَارِ وَٱكۡفُرُوٓاْ ءَاخِرَهُۥ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ
Na kikundi katika Watu wa Kitabu walisema: Yaaminini yale waliyo teremshiwa wenye kuamini mwanzo wa mchana, na yakataeni mwisho wake; huenda wakarejea.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pote la watu wa Kitabu miongoni mwa Mayahudi lilisema, «Sadikini kilichoteremshwa kwa walioamini mwanzo wa mchana na mkanushe mwisho wake. Huenda wao wakafanya shaka juu ya dini yao na wakaiacha.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس