كَيۡفَ يَهۡدِي ٱللَّهُ قَوۡمٗا كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ وَشَهِدُوٓاْ أَنَّ ٱلرَّسُولَ حَقّٞ وَجَآءَهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ
Mwenyezi Mungu atawaongoaje watu walio kufuru baada ya kuamini kwao, na wakashuhudia ya kuwa Mtume huyu ni wa haki, na zikawafikia hoja zilizo wazi? Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Vipi Mwenyezi Mungu Atawaafikia, wamuamini Yeye na wamfuate, watu walioukanusha unabii wa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, baada ya kuuamini na kushuhudia kuwa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni mkweli na yale aliyokuja nayo ni ya kweli na zikawajia wao hoja zinazotoka kwa Mwenyezi Mungu na dalili za usahihi wake? Na Mwenyezi Mungu Hawaafikii kwenye haki na usawa watu madhalimu, nao ni wale waliopotoka kwenye haki wakafuata batili, wakachagua ukafiri badala ya Imani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس