ترجمة معاني سورة الإنسان باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation


Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
آية رقم 12

Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
آية رقم 14

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
تقدم القراءة