ترجمة معاني سورة الإنسان باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
Al-Insan
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
آية رقم 2
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
آية رقم 3
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
آية رقم 4
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
آية رقم 5
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
آية رقم 6
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
آية رقم 7
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
آية رقم 8
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
آية رقم 9
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
آية رقم 10
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
آية رقم 11
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.
آية رقم 12
ﮅﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
آية رقم 13
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
آية رقم 14
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
آية رقم 15
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
آية رقم 16
ﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
آية رقم 17
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
آية رقم 18
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
آية رقم 19
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
آية رقم 20
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
آية رقم 21
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
آية رقم 22
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
آية رقم 23
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
ﰋ
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
آية رقم 24
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
آية رقم 25
ﰖﰗﰘﰙﰚ
ﰛ
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
آية رقم 26
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
آية رقم 27
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
آية رقم 28
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
آية رقم 29
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
آية رقم 30
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
آية رقم 31
Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.
تقدم القراءة