۞لَيۡسُواْ سَوَآءٗۗ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ أُمَّةٞ قَآئِمَةٞ يَتۡلُونَ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ ءَانَآءَ ٱلَّيۡلِ وَهُمۡ يَسۡجُدُونَ
Wote hao si sawa sawa. Miongoni mwa Watu wa Kitabu wamo watu walio simama baraabara, wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Waliopewa Vitabu hawako sawa: kati yao liko kundi lifuatalo njia iliyolingana sawa juu ya amri ya Mwenyezi Mungu, lenye kumuamini Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na ambalo watu wake wanasimama usiku wakizisoma aya za Qur’ani tukufu na wakielekea kwa Mwenyezi Mungu kwa kumuomba katika Swala zao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس