وَمَا يَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلَن يُكۡفَرُوهُۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ
Na kheri yoyote wanayo ifanya hawatanyimwa malipwa yake. Na Mwenyezi Mungu anawajua wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kitendo chochote, kichache au kingi, kati ya vitendo vyema yatakayofanywa na kikundi hiki kilichoamini, hakitapotea mbele ya Mwenyezi Mungu. Bali watashukuriwa na watapewa malipo yake. Mwenyezi Mungu Anawajua zaidi wacha-Mungu ambao wametenda mema na wakajitenga na yaliyoharamishwa kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kutaka thawabu Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس