وَمَآ أَصَٰبَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡتَقَى ٱلۡجَمۡعَانِ فَبِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَلِيَعۡلَمَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na yaliyo kusibuni siku yalipo pambana majeshi mawili yalikuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ili awajue Waumini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na yale yaliyotokea kwenu ya majaraha au ya mauaji katika vita vya Uhud, siku ulipokutana mkusanyiko wa Waumini na mkusanyiko wa washirikina, na ukawa ushindi, mwanzo wa vita, ni wa Waumini kisha, mara ya pili, ukwa ni wa washirikina, yote hayo yalikuwa kwa uamuzi wa Mwenyezi Mungu na mpango Wake, ili yajitokeze yale Aliyoyajua Mwenyezi Mungu tangu kale, ili Awapambanue Waumini wa kweli miongoni mwenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس