ٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلۡقَٰنِتِينَ وَٱلۡمُنفِقِينَ وَٱلۡمُسۡتَغۡفِرِينَ بِٱلۡأَسۡحَارِ
Wanao subiri, wanao sema kweli, na wat'iifu, na wanao toa sadaka, na wanao omba maghafira kabla ya alfajiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa ndio waliosifika kwa subira juu ya kumtii Mwenyezi Mungu, kuepuka maasia na juu ya shida zinazowafikia zilizokadiriwa na Mwenyezi Mungu. Na ndio waliosifika kwa ukweli wa maneno na vitendo na kutii kikamilifu. Na ndio waliosifika kwa utoaji, wa siri na wadhahiri, na kwa kuleta istighfar: kuomba msamaha, katika mwisho wa usiku, kwa kuwa wakati huo unatarajiwa zaidi kukubaliwa amali na kujibiwa dua.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس