لَّا يَتَّخِذِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ فَلَيۡسَ مِنَ ٱللَّهِ فِي شَيۡءٍ إِلَّآ أَن تَتَّقُواْ مِنۡهُمۡ تُقَىٰةٗۗ وَيُحَذِّرُكُمُ ٱللَّهُ نَفۡسَهُۥۗ وَإِلَى ٱللَّهِ ٱلۡمَصِيرُ
Waumini wasiwafanye makafiri kuwa wapenzi wao badala ya Waumini. Na anaye fanya hivyo, basi hatakuwa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Ila ikiwa kwa ajili ya kujilinda na shari zao. Na Mwenyezi Mungu anakuhadharisheni naye. Na marejeo ni kwa Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Anawakataza Waumini kuwafanya makafiri kuwa ni wategemewa, kwa mapenzi na kwa kutaka himaya, badala ya Waumini. Na yoyote mwenye kuwafanya wao ni wategemewa, huyo ameshakuwa mbali na Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu Yuko mbali na yeye. Isipokuwa mkiwa ni madhaifu wenye kuogopa, hapo Mwenyezi Mungu Amewapa ruhusa muwasairi ili kujiepusha na shari lao, mpaka mtakapopata nguvu. Na Mwenyezi Mungu Anawatahadharisha nyinyi na Yeye. basi mcheni na muogopeni. Na Kwake Peke Yake ndio marejeo ya viumbe kwa kuhesabiwa na kulipwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس