فَمَنۡ حَآجَّكَ فِيهِ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ فَقُلۡ تَعَالَوۡاْ نَدۡعُ أَبۡنَآءَنَا وَأَبۡنَآءَكُمۡ وَنِسَآءَنَا وَنِسَآءَكُمۡ وَأَنفُسَنَا وَأَنفُسَكُمۡ ثُمَّ نَبۡتَهِلۡ فَنَجۡعَل لَّعۡنَتَ ٱللَّهِ عَلَى ٱلۡكَٰذِبِينَ
Watakao kuhoji katika haya baada ya kukufikilia ilimu hii waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wake zetu na wake zenu, na sisi wenyewe na nyinyi wenyewe, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi yoyote mwenye kujadiliana nawe , ewe Mtume, kuhusu Al-Masīḥ ‘Īsā mwana wa Maryam, baada ya ujuzi uliokufikia juu ya ‘Īsā, amani imshukie, waambie, «Njooni tuwahudhurishe watoto wetu wa kiume na watoto wenu wa kiume, wanawake wetu na wanawake wenu na sisi wenyewe na nyinyi wenyewe, kisha tuelekee kwa Mwenyezi Mungu kwa kumuomba Ayashukishe mateso Yake na laana Yake juu ya warongo katika maneno yao, wenye kukamaa katika upotofu wao.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس