يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تُحَآجُّونَ فِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمَآ أُنزِلَتِ ٱلتَّوۡرَىٰةُ وَٱلۡإِنجِيلُ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Enyi Watu wa Kitabu! Mbona mnabishana juu ya Ibrahim, na hali Taurati na Injili hazikuteremshwa ila baada yake? Basi hamzingatii?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi watu wa vitabu vilivyoteremshwa, miongoni Mwa Mayahudi na Wanaswara, vipi kila mmoja kati yenu anabisha kwamba Ibrāhīm, amani imshukie, alikuwa kwenye mila yake. Ilhali Taurati na Injili hazikuteremshwa ela baada yake? Kwani hamufahamu upotofu wa maneno yenu kwamba Ibrāhīm alikuwa Myahudi au Mnaswara, na hali mnajua kuwa Uyahudi na Unaswara ulizuka baada ya kufa kwake kwa muda?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس