هَـٰٓأَنتُمۡ هَـٰٓؤُلَآءِ حَٰجَجۡتُمۡ فِيمَا لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞ فَلِمَ تُحَآجُّونَ فِيمَا لَيۡسَ لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ
Angalieni! Nyinyi mlibishana katika yale mliyo yajua. Mbona sasa mnabishana katika yale msiyo yajua? Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ndio nyinyi enyi hawa, mliomjadili Mtume wa Mwenyezi Mungu , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, juu ya mambo ya dini yenu ambayo muna ujuzi nayo, katika yale yaliyomo ndani ya vitabu vyenu mnayoitakidi usahihi wake. Lakini ni kwa nini nyinyi mnayajadili mambo ya Ibrāhīm ambayo hamuna ujuzi nayo? Na Mwenyezi Mungu Anayajua mambo pamoja na kuwa yamefichika, na nyinyi hamjui.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس