مَا كَانَ إِبۡرَٰهِيمُ يَهُودِيّٗا وَلَا نَصۡرَانِيّٗا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفٗا مُّسۡلِمٗا وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Ibrahim hakuwa Yahudi wala Mkristo, lakini alikuwa mwongofu Muislamu, wala hakuwa katika washirikina.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ibrāhīm hakuwa ni Myahudi wala Mnaswara, kwa kuwa Uyahudi haukuwa, wala Unaswara, isipokuwa baada yake. Lakini alikuwa mfuasi na mtiifu wa amri ya Mwenyezi Mungu, aliyejisalimisha Kwake, na hakuwa ni miongoni mwa washirikina.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس