إِنَّ ٱلَّذِينَ يَشۡتَرُونَ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ وَأَيۡمَٰنِهِمۡ ثَمَنٗا قَلِيلًا أُوْلَـٰٓئِكَ لَا خَلَٰقَ لَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ ٱللَّهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيۡهِمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Hakika wanao uza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapo vyao thamani ndogo, hao hawatakuwa na sehemu ya kheri yoyote katika Akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama Siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watapata adhabu chungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale ambao wanabadilisha ahadi ya Mwenyezi Mungu na wasia Wake Aliowausia katika Vitabu Alivowateremshia Mitume wao, kwa kupokea kitu kitwevu miongoni mwa vyombo vya ulimwengu na taka zake, wao hawana fungu la thawabu katika Akhera. Na Mwenyezi Mungu Hatasema na wao maneno ya kuwafurahisha; wala hatawaangalia kwa jicho la huruma Siku ya Kiyama na wala Hatawasafisha kutokana na uchafu wa madhambi na ukafiri. Na watakuwa na adhabu yenye kuumiza.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس