إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ ثُمَّ ٱزۡدَادُواْ كُفۡرٗا لَّن تُقۡبَلَ تَوۡبَتُهُمۡ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلضَّآلُّونَ
Hakika wale walio kufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, toba yao haitakubaliwa, na hao ndio walio potea.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale waliokufuru baada ya kuwa wao wameamini na wakaendelea kwenye ukafiri mpaka kufa, haitakubaliwa toba kutoka kwao mauti yakiwasimamia. Na wao ndio waliopotea njia wakakosa kuifikia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس