إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَمَاتُواْ وَهُمۡ كُفَّارٞ فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡ أَحَدِهِم مِّلۡءُ ٱلۡأَرۡضِ ذَهَبٗا وَلَوِ ٱفۡتَدَىٰ بِهِۦٓۗ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ وَمَا لَهُم مِّن نَّـٰصِرِينَ
Hakika wale walio kufuru, na wakafa hali ni makafiri haitakubaliwa kutoka kwa yeyote wao fidia ya dhahabu ya kujaza dunia nzima lau wangeli itoa. Hao watapata adhabu chungu, wala hawatakuwa na wa kuwanusuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale waliokanusha unabii wa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wakafa juu ya kumkufuru Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, haitakubaliwa kutoka kwa mmoja wao, Siku ya Kiyama, dhahabu iliyojaa ardhi iwe ni fidia ya nafsi yake kutokana na adhabu ya Mwenyezi Mungu, lau atajikomboa nayo kikweli. Wao wana adhabu yenye kuumiza; na hawana yoyote wa kuwaokoa na adhabu ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس