إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale waliojikinga na mateso ya Mwenyezi Mungu kwa kufanya yale Aliyowaamrisha na kuacha yale Aliyoyakataza, watapata kwa Mola wao huko Akhera, mabustani ya Peponi ambayo ndani yake kuna starehe za daima.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس