وَلَوۡ شِئۡنَا لَبَعَثۡنَا فِي كُلِّ قَرۡيَةٖ نَّذِيرٗا
Na tungeli taka tungeli peleka katika kila mji Mwonyaji.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau tungalitaka tungalimpeleka muonyaji katika kila mji, wa kuwalingania wao kwa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, na kuwaonya wao adhabu Yake. Lakini tumekufanya wewe, ewe Mtume, ni mwenye kupelekwa kwa watu wote wa ardhini, na tumekuamrisha wewe uwafikishie hii Qur’ani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس