إِن يَمۡسَسۡكُمۡ قَرۡحٞ فَقَدۡ مَسَّ ٱلۡقَوۡمَ قَرۡحٞ مِّثۡلُهُۥۚ وَتِلۡكَ ٱلۡأَيَّامُ نُدَاوِلُهَا بَيۡنَ ٱلنَّاسِ وَلِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَيَتَّخِذَ مِنكُمۡ شُهَدَآءَۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلظَّـٰلِمِينَ
Kama yamekupateni majaraha, basi na hao watu wengine yamewapata majaraha mfano wa haya. Na siku za namna hii tunaweletea watu kwa zamu, ili Mwenyezi Mungu awapambanue walio amini na awateuwe miongoni mwenu mashahidi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhaalimu;
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Iwapo yatawapata, enyi Waumini, majaraha au mauaji kwenye vita vya Uḥud, na mkahuzunika kwa hilo, washirikina pia walipatwa na majaraha na mauaji kama hayo katika vita vya Badr. Hizo ni siku Mwenyezi Mungu huzigeuza kati ya watu: wakati mwengine kushinda na wakati mwengine kushindwa. Kwani katika hayo kuna hekima, mpaka yadhihiri yale Aliyoyajua Mwenyezi Mungu hapo azal (kale isiyokuwa na mwanzo), ili Mwenyezi Mungu Ampambanue aliyekuwa mkweli wa Imani na asiyekuwa mkweli, na ili Awakirimu watu miongoni mwenu kwa kuwafanya wafe mashahidi. Na Mwenyezi Mungu Hawapendi waliozidhulumu nafsi zao na wakakaa kwa kuacha kupigana katika njia Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس