ٱلَّذِينَ قَالُواْ لِإِخۡوَٰنِهِمۡ وَقَعَدُواْ لَوۡ أَطَاعُونَا مَا قُتِلُواْۗ قُلۡ فَٱدۡرَءُواْ عَنۡ أَنفُسِكُمُ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Hao ndio walio waambia ndugu zao na wao wenyewe wakakaa kitako: Lau wengeli tut'ii wasingeli uliwa. Sema: Ziondoleeni nafsi zenu mauti kama mnasema kweli.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wanafiki hawa ndio wale walioketi wakawaambia ndugu zao waliopata msiba pamoja na Waislamu kwenye vita vyao na washirikina siku ya Uhud, «Lau kama watu hawa wangalitutii hawangaliuawa.» Sema, ewe Mtume, uwaambie «Zizuieni nafsi zenu na kifo, ikiwa nyinyi ni wa kweli katika madai yenu kwamba wao kama wangaliwatii hawangaliuawa na kwamba mumeokoka na mauti kwa kukaa kwenu kutokwenda vitani.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس