۞لَتُبۡلَوُنَّ فِيٓ أَمۡوَٰلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡ وَلَتَسۡمَعُنَّ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكُمۡ وَمِنَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُوٓاْ أَذٗى كَثِيرٗاۚ وَإِن تَصۡبِرُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ذَٰلِكَ مِنۡ عَزۡمِ ٱلۡأُمُورِ
Hapana shaka yoyote mtapata misukosuko katika mali zenu na nafsi zenu, na bila ya shaka yoyote mtasikia udhia mwingi kutokana na walio pewa Kitabu kabla yenu na wale walio shiriki. Na ikiwa mtasubiri na mkamchamngu basi hakika hayo ni katika mambo ya kuazimia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mtapewa mtihani, tena mtapewa mtihani, enyi Waumini, katika mali yenu kwa kutakiwa mtoe matumizi ya wajibu na yanayopendekezwa na kwa mikasa inayoyakumba. Pia mtapewa mtihani katika nafsi zenu kwa kutakiwa mtekeleze ya wajibu ya kumtii Mwenyezi Mungu na kwa misiba inayowafikia ya majaraha au mauaji na kuwakosa vipenzi vyenu. Hilo litaendelea mpaka apambanuke mwenye imani ya kweli na mwenginewe. Na mtasikia, tena mtasikia, kutoka kwa Mayahudi, Wanaswara na washirikina maneno yatakayoudhi masikizi yenu katika matamshi ya ushirikina na kuitukana dini yenu. Na iwapo mtasubiri, enyi Waumini, juu ya hayo yote na mkamcha Mwenyezi Mungu kwa kujilazimisha kumtii Yeye na kujiepusha na kumuasi, hakika hilo ni miongoni mwa mambo ambayo yanakusudiwa kidhati na kushindaniwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس