ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَٰمٗا وَقُعُودٗا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَٰذَا بَٰطِلٗا سُبۡحَٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ambao wanamtaja Mwenyezi Mungu katika hali zao zote, wakiwa wamesimama, wakiwa wameketi na wakiwa wamelala kwa mbavu zao, huku wana mazingatio juu ya uumbaji wa mbingu na ardhi hali ya kusema, «Ewe Mola wetu, Hukuuleta uumbaji huu kwa upuzi; Wewe Umetakasika na hilo! Basi tuepushie adhabu ya Moto.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس