إِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكِ بِكَلِمَةٖ مِّنۡهُ ٱسۡمُهُ ٱلۡمَسِيحُ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ وَجِيهٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kadhalika hukuwako huko, ewe Nabii wa Mwenyezi Mungu, pindi Malaika waliposema, «Ewe Maryam, Mwenyezi Mungu Anakubashiria mtoto ambaye kupatikana kwake kutatokana na neno la Mwenyezi Mungu, yaani Atamwambia, ‘Kuwa,’ na atakuwa, jina lake ni Al-Masīḥ ‘Īsā mwana wa Maryam. Yeye atakuwa na jaha katika ulimwengu na Akhera na atakuwa ni miongoni mwa wenye kukurubishwa kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس