۞وَمِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مَنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِقِنطَارٖ يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ وَمِنۡهُم مَّنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِدِينَارٖ لَّا يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ إِلَّا مَا دُمۡتَ عَلَيۡهِ قَآئِمٗاۗ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُواْ لَيۡسَ عَلَيۡنَا فِي ٱلۡأُمِّيِّـۧنَ سَبِيلٞ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ
Na miongoni mwa Watu wa Kitabu yupo ambaye ukimpa amana ya mrundi wa mali atakurudishia, na miongoni mwao yupo ambaye ukimpa amana ya dinari moja hakurudishii isipo kuwa ukimsimamia kumdai. Haya ni kwa kuwa wakisema: Hatuna lawama kwa ajili ya hawa wasio jua kusoma. Na wanamzulia uwongo Mwenyezi Mungu, hali nao wanajua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na miongoni mwa Watu wa Kitabu, katika Mayahudi, kuna ambaye lau utamuamini kwa mali mengi atakutekelezea bila hiana. Na miongoni mwao kuna ambaye lau utamuamini kwa dinari moja hatakutekelezea, mpaka ufanye juhudi kubwa ya kumfuata. Sababu ya hilo, ni itikadi mbovu inayowafanya wajihalalishie mali ya Waarabu kwa njia ya batili. Na wanasema, «Hatuna dhambi wala kosa kwa kula mali yao, kwa kuwa Mwenyezi Mungu ameyahalalisha kwetu.» Huu ni urongo wa kumzulia Mwenyezi Mungu; wanausema kwa ndimi zao na hali wanajua kuwa wao ni warongo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس