وَإِنَّ مِنۡهُمۡ لَفَرِيقٗا يَلۡوُۥنَ أَلۡسِنَتَهُم بِٱلۡكِتَٰبِ لِتَحۡسَبُوهُ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَمَا هُوَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَيَقُولُونَ هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ وَمَا هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ
Na wapo baadhi yao wanao pindua ndimi zao katika kusoma Kitabu ili mdhanie kuwa hayo yanatoka Kitabuni, na wala hayatoki Kitabuni. Na husema: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu. Na wala hayatoki kwa Mwenyezi Mungu. Na wanamsingizia Mwenyezi Mungu uwongo na wao wanajua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Miongoni mwa Mayahudi kuna watu wanaoyapotoa maneno na kuyaondoa mahali pake. Na wanayabadilisha maneno ya Mwenyezi Mungu, ili kuwafanya wasiokuwa wao wadhanie kuwa hayo ni miongoni mwa maneno yaliyoteremshwa katika Taurati, nayo si katika maneno yaliyomo kwenye Taurati kabisa, na wanasema, «Haya yanatoka kwa Mwenyezi Mungu, yameletwa kwa Nabii Wake Mūsā kwa njia ya wahyi.» Nayo hayatoki kwa Mwenyezi Mungu. Na wao, kwa ajili ya ulimwengu wao, wanasema urongo kumzulia Mwenyezi Mungu, na hali wanajua kuwa wao ni warongo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس