مَا كَانَ لِبَشَرٍ أَن يُؤۡتِيَهُ ٱللَّهُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحُكۡمَ وَٱلنُّبُوَّةَ ثُمَّ يَقُولَ لِلنَّاسِ كُونُواْ عِبَادٗا لِّي مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلَٰكِن كُونُواْ رَبَّـٰنِيِّـۧنَ بِمَا كُنتُمۡ تُعَلِّمُونَ ٱلۡكِتَٰبَ وَبِمَا كُنتُمۡ تَدۡرُسُونَ
Haiwezi kuwa mtu aliye pewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hikima na Unabii kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu. Bali atawaambia: Kuweni wenye kumuabudu Mola Mlezi wa viumbe vyote, kwa kuwa nyinyi mnafundisha Kitabu na kwa kuwa mnakisoma.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Haitakiwi kwa binadamu yoyote ateremshiwe kitabu na Mwenyezi Mungu chenye kutoa uamuzi kwa viumbe Wake na achaguliwe kuwa ni Nabii, kisha awaambie watu, «Niabuduni mimi badala ya Mwenyezi Mungu.» Lakini atasema, «Kuweni ni watu wa busara, wenye kuelewa na wajuzi wa wahyi wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, mliokuwa mkiwafundisha wengine na mnaousoma kwa kuuhifadhi, kuujua na kuuelewa..»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس