وَنَادَىٰٓ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ أَنۡ أَفِيضُواْ عَلَيۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ أَوۡ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُۚ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ حَرَّمَهُمَا عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na watu wa Motoni watawaita watu wa Peponi: Tumimieni maji, au chochote alicho kuruzukuni Mwenyezi Mungu. Nao watasema: Hakika Mwenyezi Mungu ameviharimisha hivyo kwa makafiri,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Watu wa Motoni wataomba msaada kwa watu wa Peponi wawamiminie maji au chakula Mwenyezi Mungu Alichowaruzuku. Na wao watawajibu kwamba Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ameviharamisha vinywaji na vyakula kwa walioukanusha upweke Wake na wakawafanya Mitume Wake kuwa ni warongo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس