فَلَا تَضۡرِبُواْ لِلَّهِ ٱلۡأَمۡثَالَۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ
Basi msimpigie Mwenyezi Mungu mifano. Hakika Mwenyezi Mungu anajua, na nyinyi hamjui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mjuapo kwamba masanamu na mizimu havinufaishi, basi msimfanye Mwenyezi Mungu Ana ambao ni kama Yeye wenye kufanana na Yeye miongoni mwa viumbe Wake mkawa mnawashirikisha wao pamoja na Yeye katika ibada. Hakika Mwenyezi Mungu Anayajua mnayoyafanya, na nyinyi mumeghafilika hamjui makosa yenu na ubaya wa mwisho wenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس