وَلَمَّا جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٞ لِّمَا مَعَهُمۡ نَبَذَ فَرِيقٞ مِّنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ كِتَٰبَ ٱللَّهِ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ كَأَنَّهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na alipo wajia Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, mwenye kuthibitisha yale waliyo nayo, kundi moja miongoni mwa wale walio pewa Kitabu lilitupa Kitabu cha Mwenyezi Mungu hicho nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na alipowajia Muhammad, rehema na amani zimshukie, na Qur’ani inayoafikiana na Taurati waliyonayo, kilitoka kikundi cha watu katika wao wakakitupa kitabu cha Mwenyezi Mungu, na kukiweka nyuma ya migongo yao. Hali yao ni hali ya wajinga wasiojua uhakika wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس