إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡتُمُونَ مَآ أَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡبَيِّنَٰتِ وَٱلۡهُدَىٰ مِنۢ بَعۡدِ مَا بَيَّنَّـٰهُ لِلنَّاسِ فِي ٱلۡكِتَٰبِ أُوْلَـٰٓئِكَ يَلۡعَنُهُمُ ٱللَّهُ وَيَلۡعَنُهُمُ ٱللَّـٰعِنُونَ
Hakika wale wanao ficha tuliyo yateremsha -- nazo ni hoja zilizo wazi na uwongofu baada ya Sisi kuzibainisha kwa watu Kitabuni -- hao anawalaani Mwenyezi Mungu, na wanawalaani kila wenye kulaani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale ambao wanazificha aya zilizo waziwazi, zijulishazo utume wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na yale aliyokuja nayo, nao ni wanavyuoni wa Kiyahudi na wajuzi wa Kinaswara na wengineo, miongoni mwa wafichao yalyoteremshwa na Mwenyezi Mungu, baada ya sisi kuyadhihirisha kwa watu katika Taurati na Injili, hao Mwenyezi Mungu Atawafukuza kutoka kwenye rehema Yake, na viumbe wote watawaapiza laana.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس