إِنَّمَا يَأۡمُرُكُم بِٱلسُّوٓءِ وَٱلۡفَحۡشَآءِ وَأَن تَقُولُواْ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Yeye anakuamrisheni maovu na machafu, na mumsingizie Mwenyezi Mungu mambo msiyo yajua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika Shetani anawaamuru mfanye kila sampuli ya dhambi baya linalowatia uovuni, na kila maasia yenye upeo wa uchafu, na mumzulie Mwenyezi Mungu urongo, kama kuharamisha halali na mangineyo, pasi na ujuzi wowote
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس