ذَٰلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ نَزَّلَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ ٱخۡتَلَفُواْ فِي ٱلۡكِتَٰبِ لَفِي شِقَاقِۭ بَعِيدٖ
Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu ameteremsha Kitabu kwa haki. Na wale walio khitilafiana katika Kitabu wamo katika upinzani ulio mbali na haki.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Adhabu hiyo ambayo wamestahili iwapate, ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu Ameteremsha Vitabu Vyake, kwa Mitume Wake, vikiwa ni vyenye kukusanya haki iliyo wazi, wakaikanusha haki hiyo. Na kwa hakika, wale waliohitalifiana katika Kitabu, wakaamini baadhi yake na kukanusha baadhi yake, wako katika ugonvi na mfarakano ulio mbali na uongofu na usawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس