وَإِذَا تَوَلَّىٰ سَعَىٰ فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيُفۡسِدَ فِيهَا وَيُهۡلِكَ ٱلۡحَرۡثَ وَٱلنَّسۡلَۚ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلۡفَسَادَ
Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na anapoondoka kutoka kwako, ewe Mtume, hufanya bidii na akachangamka katika ardhi ili alete uharibifu humo na kutilifisha mazao ya watu na kuua wanyama wao. Na Mwenyezi Mungu Hapendi uharibifu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس