يَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَۖ قُلۡ مَآ أَنفَقۡتُم مِّنۡ خَيۡرٖ فَلِلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِۗ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٞ
Wanakuuliza watoe nini? Sema: Kheri mnayo itoa ni kwa ajili ya wazazi na jamaa na mayatima na masikini na wasafiri. Na kheri yoyote mnayo ifanya Mwenyezi Mungu anaijua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wanakuuliza watu wako, ewe Nabii, «Ni kitu gani wakitoe, katika aina za mali zao, kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka? Na watoe kumpa nani?» Waambie, «Toeni kheri yoyote iliyo tahfifu kwenu katika aina za mali mazuri ya halali, na utoaji wenu uwe ni kwa wazazi wawili, walio karibu katika watu wenu na kizazi chenu, mayatima, mafukara na msafiri mwenye uhitaji aliye mbali na watu wake na mali yake. Na kheri yoyote mtakayoifanya, basi Mwenyezi Mungu Aliyetukuka ni mwenye kuijua.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس