إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَن تُغۡنِيَ عَنۡهُمۡ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُم مِّنَ ٱللَّهِ شَيۡـٔٗاۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ وَقُودُ ٱلنَّارِ
Kwa hakika wale walio kufuru hazitowafaa kitu kwa Mwenyezi Mungu mali zao, wala watoto wao; nao hao ndio kuni za Motoni-
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale waliokanusha Dini ya haki na wakaikataa, hayatawafaa wao mali yao wala watoto wao kuwaepushia chochote katika adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwashukia ulimwenguni, wala hayatawakinga wao na adhabu Yake Akhera. Na hawa ndio kuni za Moto Siku ya Kiyama.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس