وَلِيَعۡلَمَ ٱلَّذِينَ نَافَقُواْۚ وَقِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ قَٰتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوِ ٱدۡفَعُواْۖ قَالُواْ لَوۡ نَعۡلَمُ قِتَالٗا لَّٱتَّبَعۡنَٰكُمۡۗ هُمۡ لِلۡكُفۡرِ يَوۡمَئِذٍ أَقۡرَبُ مِنۡهُمۡ لِلۡإِيمَٰنِۚ يَقُولُونَ بِأَفۡوَٰهِهِم مَّا لَيۡسَ فِي قُلُوبِهِمۡۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يَكۡتُمُونَ
Na ili awapambanue walio kuwa wanaafiki, wakaambiwa: Njooni mpigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu au lindeni. Wakasema: Tungeli jua kuna kupigana bila ya shaka tungeli kufuateni. Wao siku ile walikuwa karibu na ukafiri kuliko Imani. Wanasema kwa midomo yao yasiyo kuwamo nyoyoni mwao. Na Mwenyezi Mungu anajua kabisa wanayo yaficha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ili Awapambanue wanafiki ambao Mwenyezi Mungu Ameyafungua wazi yaliyomo ndani ya nyoyo zao, walipokuwa Waumini wawaambia, «Njooni mpigane pamoja na sisi katika njia ya Mwenyezi Mungu au kuweni ni msaada kwetu kwa kutufanya tuwe wengi.» Wakasema, «Lau kama tunajua kuwa nyinyi mtapigana na yoyote tungalikuwa na nyinyi dhidi yao.» Wao katika ukafiri, siku hii ya leo, wako karibu zaidi kuliko kuwa wao wako karibu na Imani.Kwani wao wanayasema kwa midomo yao yasiokuwa kwenye nyoyo zao. Na Mwenyezi Mungu Anayajua zaidi wanayoyaficha vifuani mwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس