۞فَلَمَّآ أَحَسَّ عِيسَىٰ مِنۡهُمُ ٱلۡكُفۡرَ قَالَ مَنۡ أَنصَارِيٓ إِلَى ٱللَّهِۖ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ نَحۡنُ أَنصَارُ ٱللَّهِ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَٱشۡهَدۡ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ
Isa alipo hisi kuwa kati yao pana ukafiri alisema: Nani wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu? Wanafunzi wake wakasema: Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu. Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na shuhudia kwamba sisi hakika ni Waislamu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Alipohisi 'Īsā kutoka kwao ukakamavu juu ya ukafuri, aliita kwa watu wake halisi kwa kusema, «Ni nani atakayekuwa na mimi katika kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu.» Wale wasafiwa wa 'Īsā walisema, «Sisi ni wenye kuinusuru dini ya Mwenyezi Mungu na wenye kuilingania, tumemuamini Mwenyezi Mungu na tumekufuata; na ushuhudie, ewe 'Īsā, kuwa sisi tumejisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kumpwekesha na kumtii.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس