۞وَٱكۡتُبۡ لَنَا فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٗ وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِ إِنَّا هُدۡنَآ إِلَيۡكَۚ قَالَ عَذَابِيٓ أُصِيبُ بِهِۦ مَنۡ أَشَآءُۖ وَرَحۡمَتِي وَسِعَتۡ كُلَّ شَيۡءٖۚ فَسَأَكۡتُبُهَا لِلَّذِينَ يَتَّقُونَ وَيُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَٱلَّذِينَ هُم بِـَٔايَٰتِنَا يُؤۡمِنُونَ
Na utuandikie mema katika dunia hii na katika Akhera. Sisi tumerejea kwako. (Mwenyezi Mungu) akasema: Adhabu yangu nitamsibu nayo nimtakaye. Na rehema yangu imeenea kila kitu. Lakini nitawaandikia khasa wanao mchamngu, na wanao toa Zaka, na wale ambao wanaziamini Ishara zetu,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na utujaalie ni miongoni mwa wale uliowaandikia matendo mema ulimwenguni na Akhera. Sisi tumerejea kwako hali ya kutubia.» Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Akasema kumwambia Mūsā, «Adhabu yangu nitampatiliza kwayo ninayemtaka miongoni mwa viumbe wangu, kama nilivyowapatiliza hawa niliowapatia katika watu wako, na rehema yangu imewaenea viumbe wangu wote, nitawaandikia wale wanaomcha Mwenyezi Mungu na kuogopa mateso Yake, wakazitekeleza faradhi Zake na wakayaepuka mambo ya kumuasi, na wale ambao wao wanaziamini dalili za tawhīd (kumpwekesha Mwenyezi Mungu) na hoja zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس