فَلَمَّآ ءَاتَىٰهُمَا صَٰلِحٗا جَعَلَا لَهُۥ شُرَكَآءَ فِيمَآ ءَاتَىٰهُمَاۚ فَتَعَٰلَى ٱللَّهُ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Basi anapo wapa mwana mwema, wanamfanyia washirikina Mwenyezi Mungu katika kile kile alicho wapa. Mwenyezi Mungu ametukuka na huko kushirikisha kwao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Alipowaruzuku, yule mume na mke, mtoto mwema walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika katika mtoto yule ambaye Mwenyezi Mungu Alipwekeka katika kumuumba wakamfanya ni mja wa asiyekuwa Mwenyezi Mungu; Ametukukuka Mwenyezi Mungu na Ameepukana na kila mshirika.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس