وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Na tukawamiminia mvua. Basi tazama jinsi ulivyo kuwa mwisho wa wakosefu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Akawaadhibu makafiri wa kaumu ya Lūṭ, kwa kuwateremshia wao mvua ya mawe, Akaigeuza nchi yao Akaifanya juu ni chini na chini ni juu. Tazama ulivyokuwa mwisho wa wale waliojasiri kufanya matendo ya kumuasi Mwenyezi Mungu na wakawakanusha Mitume Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس