بَدِيعُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ وَإِذَا قَضَىٰٓ أَمۡرٗا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُۥ كُن فَيَكُونُ
Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ndiye Muumba mbingu na ardhi, bila ya kuwa na mfano uliotangulia. Na Anapolikadiri jambo na Akataka liwe, huliambia, “Kuwa,” likawa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس