وَٱتَّقُواْ يَوۡمٗا لَّا تَجۡزِي نَفۡسٌ عَن نَّفۡسٖ شَيۡـٔٗا وَلَا يُقۡبَلُ مِنۡهَا عَدۡلٞ وَلَا تَنفَعُهَا شَفَٰعَةٞ وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ
Na iogopeni siku ambayo hatamfaa mtu mwenziwe kwa lolote, wala hakitakubaliwa kwake kikomboleo, wala maombezi hayatamfaa, wala hawatanusuriwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ogopeni vitisho vya Siku ya Hesabu. Kwani hapo, hakuna nafsi itakayoifaa kitu chochote nafsi nyingine, wala Mwenyezi Mungu Hatakubali fidia, kutoka kwa hiyo nafsi, ya kuiyokoa na adhabu, wala hainufaiki kwa kuombewa na hakuna yoyote wa kuinusuru.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس