إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ وَأَصۡلَحُواْ وَبَيَّنُواْ فَأُوْلَـٰٓئِكَ أَتُوبُ عَلَيۡهِمۡ وَأَنَا ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ
Ila wale walio tubu na wakatengeneza na wakabainisha, basi hao nitapokea toba yao, na Mimi ni Mwenye kupokea toba na Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Isipokuwa wale waliorudi hali ya kutubia makosa yao, wakarekebisha waliyoyaharibu na wakayabainisha waliyoyaficha. Hao nitazikubali toba zao na nitawalipa kwa kuwasamehe. Na mimi ni Mwenye kukubali mno toba ya mwenye kutubia kati ya waja Wangu na ni Mwenye huruma kwao kwa kuwapa taufiki ya kutubia na kukubali toba kutoka kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس