وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱتَّبِعُواْ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ قَالُواْ بَلۡ نَتَّبِعُ مَآ أَلۡفَيۡنَا عَلَيۡهِ ءَابَآءَنَآۚ أَوَلَوۡ كَانَ ءَابَآؤُهُمۡ لَا يَعۡقِلُونَ شَيۡـٔٗا وَلَا يَهۡتَدُونَ
Na wanapo ambiwa: Fuateni aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu; wao husema: Bali tutafuata tuliyo wakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao walikuwa hawaelewi kitu, wala hawakuongoka?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pindi Waumini wasemapo, wakiwanasihi viongozi wa upotofu, «Fuateni Aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu miongoni mwa Qur’ani na uongofu,» wao huendelea kuwa wakakamavu katika kuwaigiza wakale wao washirikina, huku wakisema, «Hatufuati dini yenu, bali tunayafuata yale tuliyowakuta wazazi wetu wakiyafanya.» Wanawafuata baba zao hata kama walikuwa hawaelewi chochote kutoka kwa Mwenyezi Mungu wala hawana muelekeo wowote?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس