وَقَٰتِلُوهُمۡ حَتَّىٰ لَا تَكُونَ فِتۡنَةٞ وَيَكُونَ ٱلدِّينُ لِلَّهِۖ فَإِنِ ٱنتَهَوۡاْ فَلَا عُدۡوَٰنَ إِلَّا عَلَى ٱلظَّـٰلِمِينَ
Na piganeni nao mpaka pasiwepo fitina, na Dini iwe ya Mwenyezi Mungu tu. Na kama wakiacha basi usiweko uadui ila kwa wenye kudhulumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na endeleeni, enyi Waumini, kuwapiga vita washirikina wafanyao uadui mpaka kusiweko tena kuwafitini Waislamu na dini yao wala kumshirikisha Mwenyezi Mungu, na ibakie dini kuwa ni ya Mwenyezi Mungu Peke Yake, hali ya kuwa safi, haabudiwi yoyote pamoja na Yeye. Na iwapo watakomeka na ukafiri na vita, basi komekeni nao.Kwani mateso hayawi ela kwa wale wanaoendelea na ukafiri wao na uadui wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس