فَإِن زَلَلۡتُم مِّنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡكُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Na ikiwa mkateleza baada ya kukufikieni hoja zilizo wazi, basi jueni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na iwapo mtapondoka kwenye njia ya haki, baada ya kujiliwa na hoja wazi-wazi za Qur’ani na Suna, basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mshindi katika ufalme Wake, hakuna chochote kilicho nje ya mamlaka Yake, ni Mwingi wa hekima kwenye amri Zake na Makatazo yake, Anaweka kila kitu pahali pake palinganapo nacho.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس